Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi November 9 





 

Manchester United imeondoshwa katika Mashindano UEFA Champions League baada ya kukubali kulala kwa jumla ya mabao 2-1 ikiwa Uwanja wake wa nyumbani, Old Trafford, dhidi ya Sevilla kutoka Spain.

Mabao ya Sevilla yamefungwa na Ben Yedder katika ya 74 na 78 kipindi cha pili, huku bao la United likifungwa na Lukaku kwenye dakika ya 84.

Katika mchezo wa kwanza uliopigwa Spain, timu hizo zilenda sare ya 0-0.

Matokeo hayo sasa yanaiondosha rasmi Manchester United kwenye michuano hii na inakuwa timu ya kwanza kutoka England kutolewa mashindanoni.
Rais Donald Trump amefuta kazi Waziri wa wa Mambo ya Nje, Rex Tillerson na
amemteua Mkurugenzi wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) Mike Pompeo.

"Mike Pompeo, ambaye ni mkurugenzi wa CIA, atakuwa waziri wetu wa mambo ya nje. Atafanya kazi vizuri sana," amesema Trump kwa njia ya Twitter Jumanne.

"Nakushukuru sana Rex Tillerson kwa huduma uliyoitoa!" ameongeza rais.

Shirika la Habari la CNN limesema nafasi ya Pompeo inatarajiwa kuchukuliwa na Gina Haspel.

Tillerson, Jumatatu alilazimika kukatisha ziara yake ya kwanza ndefu barani Afrika kwa kile kilichoelezwa kwamba kazi nyingi.

“Kutokana na mahitaji katika ratiba ya waziri, anarudi Marekani mapema baada ya kukamilisha ziara ya kiserikali Chad na Nigeria,” amesema msaidizi wake Steve Goldstein.

Tillerson aliyeanza ziara ya Afrika Jumatano alirudi Marekani baada ya kutembelea Ethiopia, Djibouti na Kenya ambako ilielezwa aliugua kwa muda.

Kwa mujibu wa CNN, Trump alimtaka Tillerson kujiuzulu nafasi hiyo tangu Ijumaa wakati akiwa katika ziara ya nchi kadhaa za Afrika.
Kamanda wa Jeshi la Polisi kanda maalum DSM, Lazaro Mambosasa amesema kuwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi, Abdul Nondo hakutekwa

. Aidha amesema uchunguzi umebainisha kuwa alikwenda Mkoani Iringa kwa mpenzi wake waliyekuwa wakiwasiliana muda wote wa safari.

“Polisi baada ya kupata taarifa hii tulianza ufuatiliaji ili kubaini ukweli, tulipokea taarifa kutoka jeshi la polisi Iringa kuwa Mwanafunzi huyo alipatikana mkoani humo wilaya ya Mafinga akiendelea na shughuli zake na wala hakuripoti mahali popote” -Mambosasa

Mambosasa amesema kuwa walipomkamata walikuwa na mashaka kuwa huenda akawa amepatwa na ugonjwa wa malaria ya kichwa iliyopelekea kufanya hayo na kudai kuwa alipelekwa hospitali na kupimwa na kuonekana kuwa mzima asiye na matatizo yoyote ya kiakili.

Baraza la Wazee wa Chadema limemuomba Rais John Magufuli kukutana na  wazee ili kubadilishana nao mawazo sambamba na kumpa ushauri wa masuala mbalimbali yanayoendelea nchini.

Akizungumza leo Jumanne Machi 13, 2018 katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, katibu mkuu wa baraza hilo, Roderick Lutembeka amesema kumekuwa na mambo mengi yanayopigiwa kelele, ni vyema rais akakutana na wazee ili wamueleza mambo hayo.

“Ni lazima kama Taifa tuchukue hatua mapema kabla hatujachelewa. Rais Magufuli akubali kuitikia wito wa kukutana na wazee ambao watakuwa na ujasiri wa kumshauri ili kuepusha Taifa kuingia kwenye majanga,” amesema.

Amesema suala la wazee kukutana na rais, kimekuwa ni kilio cha muda mrefu na kwamba nchini Kenya viongozi wameweza kukaa meza moja na kumaliza tofauti zao.

“Lazima tukae tujue mustakabali wa Taifa hatuwezi kusema hakuna tatizo. Tunamtaka akutane na wazee, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa tuzungumze kwa kuwa hii ni nchi yetu wote na si ya chama kimoja,” amesema.
Pengo la pointi tatu zilizokuwa zimesalia ili kuifikia Simba kileleni iliyo nafasi ya kwanza kwenye ligi msimu huu hatimaye limezibika kufutia ushindi wa Yanga dhidi ya Stand United jioni hii.

Ikicheza kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Stand United, na kuwafanya wafikishe pointi 46 sawa na vinara Simba, ingawa wanasalia kileleni kutokana na faida ya mabao mengi ya kufunga.

Alikuwa ni Yusuph Mhilu aliyefanya kazi nzuri mapema dakika ya 6 ya mchezo, kazi iliyosababisha beki wa Stand, Ally Ally kujifunga, kufuatia kupiga krosi nzuri kulia mwa Uwanja na kuzaa bao.

Dakika ya 11, kiungo aliyewahi kuichezea Simba, Ibrahim Ajib alifunga bao la pili na kufanya ubao wa matokeo usome 2-0. Mpaka dakika 45 za kwanza zinamalizika, Yanga walikuwa mbele kwa mabao hayo mawili.

Kipindi cha pili kilipoanza, Stand walimiliki mpira kwa asilimia kubwa wakipambana kutafuta mabao, ambapo juhudi zao zilizaa matunda kwa Vitalis Mayanga kufunga katika dakika ya 83.

Ilichukua dakika mbili pekee Obrey Chirwa akaiandikia Yanga bao la 3 kwenye dakika ya 85 na kufanya mchezo uende mpaka dakika 90 na kumalizika, matokeo yakiwa ni mabao 3-1.

Matokeo hayo yameifanya Yanga ilingane kwa alama na vinara wa ligi, Simba, kwa kuwa na alama sawa ambazo ni 46, japo Simba wana mchezo mmoja mkononi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa anapokea mialiko mingi kutoka nje ya nchi lakini amesema hawezi kusafiri kwenda huko kwasababu sio jimbo lake.

Akiwa ametimiza siku 859 madarakani, Rais John Magufuli ametembelea nchi chache huenda kuliko watangulizi wake wanne.

Magufuli ametembelea Kenya, Uganda, Rwanda na Ethiopia katika kipindi chote cha utawala wake huku akitimiza miaka miwili, miezi minne na siku saba tangu aapishwe kuwa Rais wa Tanzania Novemba 5, 2015.

Huenda hilo lilimfanya jana atoe siri na sababu zinazomfanya asipende kusafiri mara kwa mara nje ya nchi.

Akiwa mjini Singida jana alikozindua kiwanda cha mafuta ya kupikia cha Mount Meru Millers Group, Rais Magufuli alisema amekataa zaidi ya mialiko 70 ya kwenda nje ya nchi kwa sababu hakuchaguliwa na Watanzania kwenda huko bali kuwatumikia.