Rais
Donald Trump amefuta kazi Waziri wa wa Mambo ya Nje, Rex Tillerson na
amemteua Mkurugenzi wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) Mike Pompeo.
"Mike
Pompeo, ambaye ni mkurugenzi wa CIA, atakuwa waziri wetu wa mambo ya
nje. Atafanya kazi vizuri sana," amesema Trump kwa njia ya Twitter
Jumanne.
"Nakushukuru sana Rex Tillerson kwa huduma uliyoitoa!" ameongeza rais.
Shirika la Habari la CNN limesema nafasi ya Pompeo inatarajiwa kuchukuliwa na Gina Haspel.
Tillerson, Jumatatu alilazimika kukatisha ziara yake ya kwanza ndefu barani Afrika kwa kile kilichoelezwa kwamba kazi nyingi.
“Kutokana
na mahitaji katika ratiba ya waziri, anarudi Marekani mapema baada ya
kukamilisha ziara ya kiserikali Chad na Nigeria,” amesema msaidizi wake
Steve Goldstein.
Tillerson
aliyeanza ziara ya Afrika Jumatano alirudi Marekani baada ya kutembelea
Ethiopia, Djibouti na Kenya ambako ilielezwa aliugua kwa muda.
Kwa
mujibu wa CNN, Trump alimtaka Tillerson kujiuzulu nafasi hiyo tangu
Ijumaa wakati akiwa katika ziara ya nchi kadhaa za Afrika.

0 comments:
Post a Comment