TCRA yataja namna waliyotumia kuzifungia simu feki


TCRa imefafanua aina ya simu zilizo fungiwa kupitia meneja wa mawasiliano wa TCRA ndungu Innocent Mungy

Tukizungumzia ambavyo vimezimwa kinachofanyika kuzifunga zile IMEI bandia ambazo kwa jana tumefanikiwa kuzifunga simu zenye IMEI zipatazo laki sita na elfu 3 kwa maana ya kwamba unakuta simu moja ina IMEI mbili kwasababu simu yenye laini mbili ina IMEI mbili sasa ziko simu zenye IMEI hadi nne‘- Innocent Mungy

Kwahiyo ambacho tumeblock jana usiku ni IMEI laki sita ikiwa ina maana ni ambazo zinatumika kwenye simu feki, modem ya internet na IPAD, sasa sisi hatuwezi kutaja idadi ya simu ngapi tumezifungia ila tunachokijua ni kwamba IMEI laki sita ndio zimefungiwa zilizopo kwenye simu‘– Innocent Mungy

‘Zoezi hili bado linaendelea ambapo sasa hivi mtambo utakuwa unahakikisha simu zinazoingia bandia zitakuwa zinafungiwa, IMEI ni namba tambulishi  kama unakumbuka tulisema kwamba kila simu inayotengezwa inapewa namba tambulishi, sasa simu ili itengenezwe lazima ipite kwenye mchakato wa kuhakikisha kuna vitu ambavyo havitakiwi viwepo kwenye simu- Innocent Mungy


0 comments:

Post a Comment