Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amesema
kuwa anapokea mialiko mingi kutoka nje ya nchi lakini amesema hawezi
kusafiri kwenda huko kwasababu sio jimbo lake.
Akiwa ametimiza siku 859 madarakani, Rais John Magufuli ametembelea nchi chache huenda kuliko watangulizi wake wanne.
Magufuli
ametembelea Kenya, Uganda, Rwanda na Ethiopia katika kipindi chote cha
utawala wake huku akitimiza miaka miwili, miezi minne na siku saba tangu
aapishwe kuwa Rais wa Tanzania Novemba 5, 2015.
Huenda hilo lilimfanya jana atoe siri na sababu zinazomfanya asipende kusafiri mara kwa mara nje ya nchi.
Akiwa
mjini Singida jana alikozindua kiwanda cha mafuta ya kupikia cha Mount
Meru Millers Group, Rais Magufuli alisema amekataa zaidi ya mialiko 70
ya kwenda nje ya nchi kwa sababu hakuchaguliwa na Watanzania kwenda huko
bali kuwatumikia.

0 comments:
Post a Comment